VIBIBI VYA NAZI

0 comments


Vipimo
 Mchele 2 Vikombe
 Tui la nazi zito  2 Vikombe
 Hamira 1 Kijiko Cha chai
 Unga wa ngano 2 Vijiko vya supu
 Iliki  Kiasi upendavyo
 Sukari Kiasi upendavyo
 Yai 1

 Vipimo vya Tui la Kupaka
 Tui la nazi  2 Vikombe
 Hiliki ya unga Kiasi upendacho
Sukari Kiasi upendacho
Unga wa ngano 1 Kijiko cha supu
Namna ya Kutayarisha na Kupika

  •        Changanya vitu vyote vya tui la kupaka katika kisufuria kidogo.
  •       Lipike tui huku walikoroga mpaka lichemke na liwe zito. 
  •        Osha na loweka mchele usiku mzima ndani ya maji baridi.
  • .      Mimina vifaa vyote isipokuwa yai na sukari , ndani ya mashine ya kusagia (blender) na usage mpaka mchele uwe laini.
  • .      Mimina sukari na yai usage kidogo tu kiasi cha kuchanganya.  
  • .      Mimina ndani ya bakuli na ufinike , kisha weka pahali penye joto ili mchanganyiko ufure/uvimbe
  • .      Ukishafura, weka chuma kipate moto. (Ni bora kutumia kichuma kidogo)
  • .      Katika sahani ya kupakulia, paka tui kote.
  • .      Tia kijiko nusu cha chai cha mafuta au samli kwenye chuma kisha mimina mchanganyiko ukitumia upawa na ufunike.
  • .   Kibibi kikianza kuiva na kushikana upande mmoja , kigeuze upande wa pili mpaka kigeuke rangi na kuiva.
  • .   anga kwenye sahani iliyopakwa tui.
  •   nelea Mpaka umalize mchanganyiko wote; kila ukiepua kibibi, panga juu ya mwenzake kama ilivyo kwenye picha na  upake tui juu yake.
<




Post a Comment